Exodus 38:9-14

9 aKisha akatengeneza ua. Upande wa kusini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja,
Dhiraa 100 ni sawa na mita 45.
na ulikuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri,
10pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo. 11Upande wa kaskazini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.

12Upande wa mwisho wa magharibi ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini
Dhiraa 50 ni sawa na mita 22.5.
na ulikuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
13Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, pia ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini. 14Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano
Dhiraa 15 ni sawa na mita 6.75.
yalikuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
Copyright information for SwhKC